Posts

Showing posts with the label Intelijensia

MAREKANI YAFANYIWA UJASUSI NA 'CHINA’

Image
 China imedukua kampuni nane kuu za mawasiliano za Marekani, zikiwemo AT&T, Verizon, na Lumen Technologies, ikiwapa maafisa wa Beijing uvujaji wa meseji za   siri za kampuni na binafsi katika simu nyingi  za Wamarekani, Washington imesema. Maafisa wa Marekani wamewashauri raia kutumia programu za ujumbe zilizodhibitiwa ili kupunguza hatari ya mawasiliano yao kuingiliwa.  Hata hivyo, Ikulu ya White House imebainisha kuwa mawasiliano ya siri bado hayajaathiriwa.Afisa mmoja amesema kuwa, ingawa si kila simu imeathiriwa, China ililenga idadi kubwa ya watu.  Afisa wa usalama wa mtandao Jeff Greene amesema wigo wa udukuzi ni mkubwa sana na “haiwezekani kutabiri mwisho wake.” Ikulu ya White House imeweka suala hilo kuwa kipaumbele, huku Rais Biden akipewa taarifa mara kadhaa.  Ubalozi wa China mjini Washington umekataa shutuma hizo, lakini kampeni hiyo ya udukuzi, inayodaiwa kufanywa na kikundi cha Kimbunga cha Chumvi, inatajwa kuwa mojawapo ya matukio makubwa...

JIFUNZE KUSAMEHE

Image
*_JE WAJUA?_* Kama ulikua huijui ndege ya LIBYA iliokuwa iende UGANDA kumsaidia Iddi Amini kwenye Vita vya KAGERA lakini ikapotezwa njia na kutua TANZANIA wacha nikufahamishe""      Ilikuwa mwaka 1978-1979 majasusi wa Tanzania wakiongozwa na wataalamu wa mbinu, Meja Jeneral Kiwelu akiongoza Idara ya Usalama na Utambuzi Jeshini (MI) na Hassy Kitine akiongoza Tawi Maalumu la Ujasusi Tanzania (leo TISS), waliziongoza medani za vita nchini Uganda.     Wakati vita imepamba moto, Iddi Amini Dada wa Uganda aliomba msaada wa kijeshi kutoka Libya ambapo Rais Muammar Gadaffi alimsaidia askari, vifaru na makombora ya kisasa.     Taarifu za msaada wa kijeshi wa Libya ziliifikia Idara ya Ujasusi wa Kijeshi nchini Tanzania, iliyokuwa chini ya Meja Jenerali Kiwelu, wakati huo.    Hakukuwa na chaguo zaidi ya kukabiliana na hali hiyo.     Majasusi wa Tanzania, kwa kutumia wale waliopandikizwa kwenye uwanda wa mawasiliano eneo la maziwa mak...