Posts

Showing posts with the label Matukio

WATOTO WA MAREHEMU MEJA JENERALI MBUGE WADAI HAKI ZAO KWA TRA NA BRELA

  Watoto watatu wa Marehemu Meja Jenerali Charles Mang’era Mbuge (Mstaafu) wameandika barua rasmi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), wakidai haki yao ya kisheria baada ya kifo cha baba yao. Watoto hao, Imani Charles Mbuge, Elizabeth Charles Mbuge, na Marietha Charles Mbuge, wanataka mamlaka hizo kufunga “TIN” namba na leseni za marehemu baba yao kwenye mali zilizopo Kitunda Relini, Dar es Salaam, na Kisarawe, Pwani. Kwa mujibu wa barua yao, mali zinazohusika ni Jakicha Motel , iliyopo Kitunda Relini, Dar es Salaam, na shamba la biashara lililopo Kisarawe, Pwani. Wamedai kuwa tangu kifo cha baba yao, kilichotokea tarehe 12 Oktoba 2024 katika Hospitali ya Apollo nchini India, hawajapokea mgao wowote wa fedha licha ya marehemu kuwa na umiliki wa asilimia 80 ya hisa katika Jakicha Motel. Watoto hao wametoa muda wa siku mbili, hadi kufikia tarehe 1 Januari 2025, kwa mamlaka zinazohusika kuhakikisha wanapokea kiasi cha shilingi m...

MADEREVA WAZEMBE 16,324 WAKAMATWA WAKATI WA SIKUKUU YA KRISMASI

Image
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limefanikiwa kuwakamata madereva 16,324 waliobainika kukiuka sheria za usalama barabarani katika operesheni maalum zilizofanyika wakati wa sikukuu ya Krismasi. Makosa yaliyojitokeza zaidi ni mwendo kasi, ulevi wakati wa kuendesha, kutovaa mikanda ya usalama, pamoja na magari mabovu yasiyokidhi viwango vya usalama. Operesheni hizi zililenga kupunguza ajali na kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara katika kipindi hiki cha sikukuu. Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, ACP Ramadhani Ng’anzi, amesema operesheni zitandelea katika msimu mzima wa sikukuu ili kuhakikisha madereva wanazingatia sheria na kanuni za usalama barabarani. Ameonya kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya madereva wanaopuuza sheria, kwani uzembe wao unaweza kusababisha madhara makubwa kwa jamii. Aidha, Kamanda Ng’anzi ametoa wito kwa madereva na abiria kufuata sheria na kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola ili kulinda maisha yao na ya watumiaji wengine wa barabara. Jeshi la Poli...

IGP WAMBURA KATIKA MABADILIKO YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

Image
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura, amemhamisha aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ramadhani Ng’anzi, kufuatia ongezeko la ajali za barabarani zilizoshuhudiwa mwezi Desemba 2024. Katika mabadiliko hayo yaliyotangazwa Disemba 22, 2024, DCP Ng’anzi amepelekwa Makao Makuu ya Upelelezi Dodoma, ambako atakuwa Mkuu wa Kitengo cha Makosa ya Maadili ya Jamii. Nafasi yake imechukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) William Mkonda, aliyekuwa Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Aidha, aliyekuwa Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Boniphace Mbao, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Mabadiliko haya yamefanyika wakati ambapo kumekuwa na ongezeko la ajali mbaya za barabarani nchini, hasa katika kipindi cha mwisho wa mwaka kinachoambatana na msongamano wa magari na harakati nyingi za wananchi. Akizungumza baada ya kutan...

SERIKALI YAKABIDHI NYUMBA 109 KWA WAATHIRIKA WA MAPOROMOKO HANANG

Image
SERIKALI YAKABIDHI NYUMBA 109 KWA WAATHIRIKA WA MAPOROMOKO HANANG Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo, Disemba 20, 2024, imekabidhi rasmi nyumba 109 kwa waathirika wa maporomoko ya tope yaliyotokea Disemba mwaka jana wilayani Hanang, mkoani Manyara. WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekabidhi nyumba hizo kwa waathirika wa maafa ya maporomoko ya tope yaliyotokea Desemba, mwaka jana wilayani Hanang, mkoani Manyara.   Akizungumza mara baada ya kukabidhi na kuzindua nyumba hizo zilizojengwa katika kitongoji cha Waret, Wilaya ya Hanang, mkoani Manyara, Waziri Mkuu amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anawapa pole waathirika wote na amesisitiza kuwa Serikali itawasaidia ili waendelee na maisha yao kama ilivyokuwa awali.   Amesema kuwa ujenzi wa nyumba 73 kati ya 109 umegharamiwa na Serikali Kuu na kujengwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA-JKT); nyumba nyingine 35 zimejengwa na Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania, ilhali nyumba mo...

DK. SAMIA ASIKITISHWA NA AJALI YA MIKESE, MOROGORO

Image
📌Asisitiza maelekezo aliyotoa Disemba 4, 2024 kufuatwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameonesha masikitiko makubwa kufuatia ajali mbaya iliyotokea usiku wa kuamkia leo, Desemba 18, 2024, ambapo watu 15 wamepoteza maisha na wengine kujeruhiwa. Ajali hiyo ilihusisha lori la mizigo na gari la abiria aina Coaster katika eneo la Mikese, Barabara Kuu ya Morogoro - Dar es Salaam. Dk. Samia ametoa pole kwa familia za marehemu, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mheshimiwa Adam Malima, pamoja na ndugu, jamaa, na marafiki wa waathirika. “Ninawaombea kwa Mwenyezi Mungu ndugu zetu hawa wapumzike kwa amani, na majeruhi wote wapone kwa haraka,” amesema Rais. Akirejelea maelekezo aliyoyatoa Desemba 4, 2024, kuhusu kuongeza usimamizi wa Sheria za Usalama Barabarani, Dk. Samia amesema leo ameagiza Jeshi la Polisi kutekeleza hatua mpya kwa ajili ya kuimarisha usalama barabarani. Miongoni mwa hatua hizo ni kuanzishwa kwa mfumo wa Leseni za Udereva za Elektroniki, ambao uta...

WATU 14 WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 8 WAJERUHIWA KWA AJALI

Image
  Watu 14 wamefariki dunia na wengine 8 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha lori la mizigo lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Morogoro na coaster iliyokuwa inatokea Morogoro kwenda Dar usiku wa kuamkia leo, eneo la Mikese, barabara kuu ya Morogoro - Dar es Salaam. Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, Nkungu Daniel, amethibitisha kupokea miili ya marehemu na majeruhi, na kusema kwamba miili ya waliokufa bado haijatambuliwa. Alisema kuwa kati ya waliokufa, wanaume ni 8 na wanawake ni 6, huku majeruhi wakipatiwa matibabu katika hospitali hiyo. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, alitembelea hospitali hiyo alikozuiliwa majeruhi, na aliwataka wananchi kufika hospitalini hapo ili kutambua miili ya ndugu zao waliopoteza maisha. Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa jamii katika kutambua miili na kusaidia familia za waathirika. Ajali hiyo ilihusisha madereva wawili, ambao kwa bahati mbaya walipoteza maisha.

KANISA KUU LA NOTRE DAME LAFUNGULIWA RASMI HUKO PARIS, UFARANSA

Image
Kanisa Kuu la kihistoria la Notre Dame limefunguliwa rasmi Desemba 7, 2024 jijini Paris, Ufaransa, baada ya miaka mitano ya ukarabati kufuatia moto mkubwa ulioteketeza sehemu kubwa ya jengo hilo mwaka 2019.  Hafla ya ufunguzi huo imehudhuriwa na viongozi wa kimataifa, wakiwemo Rais wa Mteule wa Marekani Donald Trump, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, pamoja na wageni mashuhuri kutoka sehemu mbalimbali duniani. Ufunguzi huu umekuwa tukio muhimu linalodhihirisha urejeshaji wa urithi wa kihistoria wa Ufaransa.  Kazi ya ukarabati wa kanisa hilo ilihusisha maelfu ya mafundi stadi, wasanifu, na wahandisi, ambao walihakikisha jengo hilo linarejeshwa kwa mwonekano wake wa awali bila kupoteza thamani yake ya kihistoria. Kanisa hilo, ambalo ni mojawapo ya alama kuu za utamaduni wa Ufaransa na kivutio cha mamilioni ya watalii kila mwaka, sasa limefunguliwa kwa ajili ya waumini na wageni wanaotaka kulishuhudia baada ya kazi kubwa ya ukarabati kukamilika.  

PUTIN NA XI JINPING WAKITENGENEZA PANCAKES PAMOJA MWAKA WA 2018

Image
Katika tukio lisilo la kawaida lakini lenye kushangaza, Rais wa Urusi, Vladimir Putin, na Rais wa China, Xi Jinping, walikutana mnamo mwaka wa 2018 na kushiriki kutengeneza pancakes. Tukio hilo lilifanyika wakati wa jukwaa la kiuchumi la mashariki (Eastern Economic Forum) huko Vladivostok, Urusi. Marais hao wawili walionekana wakitengeneza pancakes kwa ustadi huku wakijadili masuala ya kimataifa. Tukio hili lilionyesha urafiki na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika mazingira yasiyo rasmi. Pancakes walizotengeneza ziliambatana na caviar, sour cream, na asali, vyote vikiwa ni bidhaa za jadi za Urusi. Matukio kama haya yanalenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia.

SHULE HII AUSTRALIA HURUHUSU WANAFUNZI KUVUTA SIGARA SHULENI

Image
Chuo cha Arethusa College, Queensland, Australia, kimezua mjadala kwa kuruhusu wanafunzi kuchukua mapumziko ya kuvuta sigara shuleni.  Taarifa zinaonyesha kuwa karibu wanafunzi 50 hutumia eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya kuvuta sigara, hatua ambayo shule inadai husaidia kudhibiti uraibu wao na kuzuia athari mbaya kwa masomo yao. Uongozi wa shule unasema hatua hiyo inalenga kuzuia tabia hatarishi kama kuruka shule au kuvuta sigara kwa siri. Ingawa wanadai kupata kibali cha wazazi, baadhi ya wazazi wameonyesha wasiwasi, wakidai kuwa hatua hiyo imesababisha watoto wao kuanza kuvuta sigara. Arethusa College ni shule inayolenga wanafunzi waliotatizika katika mfumo wa kawaida wa elimu, lakini sera hii imeibua mjadala mkubwa kuhusu jukumu la shule katika malezi bora ya wanafunzi.

BINTI ANAYEDAIWA KUWA WA PUTIN ABADILI JINA LAKE AKIWA PARIS

Image
Binti anayedaiwa kuwa mtoto wa Rais Vladimir Putin, aliyezaliwa kutokana na uhusiano wake na msafishaji wa zamani Svetlana Krivonogikh, amekuwa akiishi Paris kwa jina tofauti na anafanya kazi kama DJ.  Binti huyo, Luiza Rozova (au Elizaveta Olegovna Rudnova), mwenye umri wa miaka 21, alifuatiliwa na vyombo vya habari vya Ukraine kupitia rekodi za ndege zilizovuja.  Inadaiwa kwamba Rozova ameacha jina lake la patronymic “Vladimirovna” na kutumia jina la “Olegovna”, ikiwa ni kiashiria cha uhusiano wake na rafiki wa karibu wa Putin aliyeaga dunia, Oleg Rudnov. Rozova alizaliwa Machi 3, 2003, na jina la babake halikuorodheshwa kwenye cheti chake cha kuzaliwa.  Anadaiwa kuwa mtoto wa uhusiano wa siri kati ya Putin na Krivonogikh, msafishaji wa zamani ambaye sasa ni miongoni mwa wanawake matajiri zaidi nchini Urusi.  Krivonogikh ni mjumbe wa bodi ya Bank Rossiya, inayotumiwa na wasomi wa Urusi kuhamisha pesa.  Kulingana na uchunguzi wa 2020 wa kundi la uchunguzi la Ur...

SHUGHULI ZA UOKOZI KARIAKOO KUHITIMISHWA LEO

Image
 Ni siku ya 10 sasa tangu maafa yatokee ya kuporomoka kwa jengo katika soko la biashara la kimataifa kariakoo asubuhi ya jumamosi tarehe 16 Novemba 2024 na kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali. Serikali imekuwa ikishughulikia maafa hayo kwa kuokoa watu, kutibu  majeruhi na kuzika waliopoteza maisha katika  maafa hayo ambapo kufikia  leo Jumanne, Novemba 26, 2024, Msemaji Mkuu wa Serikali, Thobias Makoba akizungumza na waandishi wa habari akiwa katika eneo la jengo lilipoporomoka amesema amesema shughuli ya uokozi imefikia tamati leo Jumanne Novemba 26.

ZIARA YA KIKAZI POLISI USALAMA WA RAIA

Image
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) John Imori tarehe 22 Novemba 2024 alitembelea  Wilaya ya Nachingwea ikiwa ni ziara ya kawaida ya kazi. Aidha ACP Imory alitembelea ofisi ya upelelezi wa makosa ya jinai na kuzungumza na Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai Wilaya Nachingwea ASP Fanuel Milinga. Jeshi la Polisi Tanzania limekuwa na utaratibu wa kutembelea sehemu mbali mbali katika kuimarisha usalama wa raia nchini.

POLISI MSUMBIJI WAKABILIANA NA WAANDAMANAJI BAADA YA UCHAGUZI WENYE UTATA

Image
 Polisi wa Msumbiji jana wamelazimika kurusha mabomu ya moshi (machozi) na risasi kwa waandamanaji katika mji mkuu Maputo waliokuwa wamekusanyika katika eneo la tukio ambapo viongozi wawili wa vyama vya upinzani waliuawa kwa kupigwa risasi siku ya Jumamosi baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata.  Katika maandamano hayo polisi wameonekana wakiwatawanya umati. Adriano Nuvunga, Mkurugenzi wa Kituo cha Demokrasia na Haki za Kibinadamu cha Msumbiji, amesema kuwa waandishi wa habari wawili na mlinzi mmoja walipigwa na risasi lakini hawakujeruhiwa vibaya. Msemaji wa polisi hakuweza kupatikana mara moja kuzungumzia hilo. Matokeo kamili ya uchaguzi wa kitaifa wa Oktoba 9 yanatarajiwa kutangazwa wiki hii, huku matokeo ya mapema yakionyesha kuwa chama tawala cha Frelimo kinatazamiwa kupata ushindi mwingine.  Frelimo imetawala nchi hiyo ya kusini mwa Afrika tangu mwaka 1975. Mgombea huru wa urais Venancio Mondlane alisema kuwa mgomo wa kitaifa wa Jumatatu ulizingatiwa vyema na kuwaamb...

Kuagwa kwa Mwili wa Dk. Mwele Malecela leo

Image
1. Mamia ya waombolezaji katika Jiji la Dar es Salaam wakiongozwa na viongozi mbalimbali akiwemo Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania  Kassim Majaliwa wameongoza ibada ya kuaga mwili wa Dk.Mwele Malecela. Dk.Mwele ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela ameagwa jana Februari 19, 2022 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kabla ya kupelekwa jijini Dodoma kwa ajili ya kuupumzisha mwili wake katika nyumba yake ya milele. Dk Mwele (58) aliyekuwa Mkurugenzi wa Magonjwa yasiyopewa vipaumbele Shirika la Afya Duniani(WHO) alifariki dunia Februari 10 mwaka huu Mjini Geneva ,Uswiz alipokuwa akipatiwa matibabu.