SHUGHULI ZA UOKOZI KARIAKOO KUHITIMISHWA LEO
Ni siku ya 10 sasa tangu maafa yatokee ya kuporomoka kwa jengo katika soko la biashara la kimataifa kariakoo asubuhi ya jumamosi tarehe 16 Novemba 2024 na kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali.
Serikali imekuwa ikishughulikia maafa hayo kwa kuokoa watu, kutibu majeruhi na kuzika waliopoteza maisha katika maafa hayo ambapo kufikia leo Jumanne, Novemba 26, 2024, Msemaji Mkuu wa Serikali, Thobias Makoba akizungumza na waandishi wa habari akiwa katika eneo la jengo lilipoporomoka amesema amesema shughuli ya uokozi imefikia tamati leo Jumanne Novemba 26.

Comments