Posts

Showing posts with the label Elimu

RAIS SAMIA AZINDUA SERA MPYA YA ELIMU, AZITAKA WIZARA HUSIKA KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WAKE

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa uwepo wa Sera Mpya ya Elimu na Mitaala Mipya pekee haviwezi kuleta matokeo chanya bila utekelezaji makini. Akizungumza Februari 1, 2025, jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 – Toleo la 2023, Rais Samia ameagiza wizara husika kuhakikisha kuwa utekelezaji wa sera hiyo unafanyika kikamilifu ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa. “Naitaka Wizara ya Fedha, Wizara ya Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na TAMISEMI kuwezesha na kusimamia utekelezaji wa sera na mitaala hii mpya kwa ufanisi,” amesema Rais Samia. MAGEUZI KATIKA SEKTA YA ELIMU Katika hotuba yake, Rais Samia amesisitiza kuwa maboresho hayo lazima yawazingatie walimu kwa kuwapatia mafunzo sahihi, kuwaajiri wenye sifa stahiki, na kuboresha maslahi yao. Aidha, ameweka wazi kuwa dhamira ya mabadiliko haya ni kumuandaa kijana mwenye kujiamini na aliye tayari kushindana katika soko la...

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA YAWAFIKIA WANANCHI 775,119 BAADA YA KUFIKA KIGOMA, KATAVI NA MTWARA

Image
Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imezinduliwa rasmi katika mikoa ya Kigoma, Katavi, na Mtwara, ikilenga kutoa elimu ya kisheria na msaada kwa wananchi ili kutatua changamoto zao za kisheria na kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wote. Mkoani Kigoma, Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, aliongoza uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Mwanga Centre tarehe 24 Januari 2025. Waziri Ndumbaro alisisitiza kuwa kampeni hii inalenga kulinda misingi ya kisheria na kutoa suluhisho kwa migogoro ya wananchi. Aidha, alitoa wito kwa wananchi wa Kigoma kuitumia fursa hiyo katika halmashauri zote nane za mkoa huo kwa siku tisa, huku akiwataka wasaidizi wa msaada wa kisheria kuwasaidia wananchi kwa weledi. Mkoani Katavi, Mkuu wa Mkoa, Mhe. Mwamvua Mrindoko, alitoa wito kwa viongozi wa wilaya na maafisa wa halmashauri kuhakikisha kampeni inawafikia watu wengi zaidi. Uzinduzi uliofanyika katika uwanja wa Kashaulili, Manispaa ya Mpanda, uliweka msisitizo kwenye elimu kwa wanafun...

WAVULANA WAONGOZA UFAULU KIDATO CHA NNE, WANAFUNZI 450 KURUDIA MITIHANI 2025

Image
  Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa Kidato cha Nne wa mwaka 2024, ambapo asilimia 92.37 ya watahiniwa wamefaulu. Hii ni ongezeko la ufaulu kwa asilimia 3 ikilinganishwa na mwaka 2023, ambao ulikuwa na ufaulu wa asilimia 89.36. Katika matokeo haya, jumla ya watahiniwa 477,262 kati ya 516,695 waliofanya mtihani huo wamepata madaraja ya I, II, III, na IV. Kwa upande wa jinsia, wasichana wameongoza kwa idadi ya waliofaulu, wakiwa ni 249,078 sawa na asilimia 52, huku wavulana wakiwa ni 228,184 sawa na asilimia 48. Hata hivyo, wavulana wameongoza kwa ubora wa ufaulu, ambapo asilimia 54 ya waliofaulu kwa madaraja ya I hadi III ni wavulana (119,869), ikilinganishwa na asilimia 46 ya wasichana (102,084). Aidha, NECTA imetangaza kuwa wanafunzi 450 ambao matokeo yao yamezuiwa kwa sababu mbalimbali, ikiwemo udanganyifu na changamoto nyingine, wamepewa fursa ya kurudia mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2025. NECTA imetoa wito kwa wanafunzi waliokosa uf...

WAZIRI CHANA ASISITIZA UTEKELEZAJI WA SHERIA KATIKA UWEKEZAJI WA UWINDAJI WA KITALII

Image
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) ameitaka menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya Serikali katika uwekezaji kwenye vitalu vya uwindaji kwa maslahi mapana ya Taifa. Ameyasema hayo Januari 18,2025 katika kikao kilichofanyika ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dodoma. “Hakikisheni maeneo yenye vitalu vya uwindaji wa kitalii yanakuwa salama yasivamiwe na mifugo ili wawekezaji waweze kuona thamani ya uwekezaji wao na pia ili kuongeza idadi ya wageni wanaokuja kuwinda” amesisitiza Mhe. Chana. Kikao hicho kiliambatana na kupitia taarifa mbalimbali za uwekezaji kwenye maeneo ya uwindaji wa kitalii. Kikao hicho kimehudhuriwa na Kaimu Kamishna Uhifadhi TAWA, Bw. Mlage Kabange, Kaimu Mkurugenzi wa Wanyamapori, Dkt. Fortunata Msoffe na baadhi ya watumishi waandamizi kutoka TAWA.  

RAIS MWINYI: KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI NDIYO CHACHU YA MAENDELEO ZANZIBAR

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kwamba Zanzibar inaweza kupiga hatua kubwa zaidi za maendeleo endapo kasi iliyopo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo itaendelezwa. Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo tarehe 11 Januari 2025, alipokuwa akifungua rasmi Skuli ya Msingi ya Michakaini, iliyopo Wilaya ya Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba. Aidha, Rais Dk. Mwinyi alibainisha kuwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo, hususan katika sekta za miundombinu ya barabara, masoko, na ujenzi wa skuli za ghorofa, unapaswa kuigwa na kuendelezwa kwa kasi katika sekta nyingine zote. Alisisitiza kuwa mafanikio haya yamejidhihirisha kupitia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambayo Serikali imeitekeleza kwa mafanikio makubwa, na hata kuvuka malengo yaliyowekwa ndani ya kipindi cha miaka minne ya uongozi wake. Akizungumzia skuli hiyo ya Michakaini, Rais Dk. Mwinyi alisema ujenzi huo ni hatua muhimu katika kuboresha mazingira ya wanafunzi kuso...

RAIS DKT. SAMIA AFUNGUA SHULE YA SEKONDARI MISUFINI ZANZIBAR

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 8 Januari 2025, amefungua rasmi Shule ya Sekondari ya Misufini, iliyoko Bumbwini, Zanzibar. Hafla hiyo ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea maadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Skuli ya Sekondari Misufini, iliyoko Bumbwini, Zanzibar, imejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 2.5 . Shule hii ina madarasa 12 ya kisasa, maabara tatu za masomo ya sayansi, na maktaba yenye vifaa vya kujifunzia kwa teknolojia ya kisasa. Kwa sasa, shule hii imeandikisha wanafunzi 450 , huku ikiwa na uwezo wa kuchukua hadi wanafunzi 600 katika siku zijazo. Mradi huu ni sehemu ya juhudi za serikali ya Zanzibar kuboresha elimu kwa kuwekeza katika miundombinu bora na kuongeza upatikanaji wa elimu bora kwa watoto wa Kizanzibari. Rais Samia alibainisha kuwa shule kama hii zitachangia kuinua kiwango cha elimu kwa vijana, ambao ni msingi wa maendeleo ya taifa. Katika hotuba yake, Rais Samia amesisitiza dhamira ya serika...

SEQUIP KUWANOA WALIMU 40,000 WA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI

Image
  Serikali kupitia Mradi wa Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) imeendelea kutoa mafunzo kwa walimu wa sekondari wanaofundisha masomo ya sayansi na hisabati 40,000 ili kuwapatia mbinu, maudhui na matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji shuleni.   Mradi wa SEQUIP unatekelezwa kwa pamoja kati ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na unalenga  kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita kwa muda wa miaka mitano kuanzia 2021 hadi 2026. Akifungua mafunzo hayo ya siku tano kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Atupele Ambwene katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera leo Januari 6, 2025, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu na Usimamizi wa Elimu Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Emmanuel Shindika amesema mafunzo hayo yataimarisha mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji wa masomo ya sayansi kwa wanafunzi na walimu pamoja na Wathibiti ubora kufanya tathmin...

NECTA YAFICHUA UDANGANYIFU WA MITIHANI, WACHUKUA HATUA KALI

Image
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mitihani ya darasa la nne na kidato cha pili, huku likichukua hatua kali dhidi ya vitendo vya udanganyifu vilivyobainika katika mitihani hiyo.  Matokeo ya Darasa la Nne: Katika mtihani wa darasa la nne, wanafunzi 1,320,227 kati ya 1,530,911 waliofanya mtihani huo, sawa na asilimia 86.24, wamefaulu kwa kupata madaraja A, B, C, na D. Hii ni ongezeko la asilimia 2.9 ikilinganishwa na mwaka uliopita. Kati ya waliofaulu, wasichana ni 699,901 na wavulana ni 620,326. Matokeo ya Kidato cha Pili: Kwa upande wa kidato cha pili, wanafunzi 680,574 kati ya 796,825, sawa na asilimia 85.41, wamefaulu na kuendelea na kidato cha tatu. Hii ni ongezeko la asilimia 0.10 ikilinganishwa na mwaka uliopita. Kati ya waliofaulu, wasichana ni 367,457 na wavulana ni 313,117. Udanganyifu na Hatua Zilizochukuliwa: NECTA imebaini vitendo vya udanganyifu vilivyofanywa na baadhi ya walimu na wanafunzi. Walimu katika Shule ya Msingi Bwisya (Ukerewe, Mwanza)...

TAARIFA KUHUSU USAILI WA KADA ZA UALIMU

Image
Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira inawatangazia waombaji kazi wa Kada za Ualimu kuwa usaili utaanza 14 Januari 2025 hadi 24 Februari 2025. MUHIMU: • Ratiba ya Usaili: Tovuti www.ajira.go.tz. • Eneo la Usaili: Katika mikoa wanayoishi waombaji. Kuhusu Nyaraka: Vyeti vya taaluma na kuzaliwa. • Kitambulisho halali kama NIDA au hati ya kusafiria. • Mwisho wa Kuhakiki Makazi: 06 Januari 2025, kupitia Ajira Portal. Kwa maelezo zaidi, tembelea tovuti au wasiliana na ofisi husika.  

RAIS PUTIN ATIA SAINI SHERIA YA KUPIGA MARUFUKU WATOTO WAHAMIAJI WASIOZUNGUMZA KIRUSI KUHUDHURIA SHULE

Image
Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ameidhinisha rasmi sheria inayopiga marufuku watoto wa wahamiaji wasioweza kuzungumza Kirusi kujiunga na shule za Urusi. Sheria hii inalenga kuimarisha ushirikiano wa wahamiaji katika jamii ya Urusi na kuhakikisha kuwa watoto wote wanapata elimu bora kwa kutumia lugha ya taifa. Kwa mujibu wa sheria hii, watoto wa wahamiaji ambao hawana ufanisi katika lugha ya Kirusi hawataruhusiwa kujiunga na shule za Urusi. Hii inatokana na hoja kwamba walimu wengi hawana ujuzi wa lugha za asili za wahamiaji, na hivyo inakuwa vigumu kwa watoto hao kufuata mtaala wa elimu. Hata hivyo, hatua hii imekosolewa na makundi ya kutetea haki za binadamu, ambayo yanadai kuwa sheria hii itakuwa kikwazo kwa watoto wa wahamiaji katika kupata elimu na kuungana na jamii ya Urusi. Wakosoaji wanasisitiza kuwa watoto wanapaswa kuwa na haki ya kupata elimu bila kujali ujuzi wao wa lugha. Rais wa Duma ya Jimbo, Viacheslav Volodin, ameunga mkono sheria hii na kusema kuwa familia za wahamiaji ...

BILIONI 33.4 KUKOPESHWA KWA ELIMU YA JUU ZANZIBAR

Image
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar (ZHELB), imetenga jumla ya Shilingi bilioni 33.4 kwa mwaka wa masomo 2024/2025 kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu. Kati ya fedha hizo, Shilingi bilioni 20.4 zitatumika kugharamia masomo ya wanafunzi wanaoendelea, huku Shilingi bilioni 13 zikielekezwa kwa wanafunzi wapya. Mikopo hii inalenga kugharamia ada za masomo, posho ya chakula na malazi, pamoja na posho ya vitabu na vifaa vya kujifunzia. Kwa mwaka huu, jumla ya wanafunzi 5,000 wanatarajiwa kunufaika, wakiwemo wanafunzi 3,000 wanaoendelea na wanafunzi wapya 2,000. Hii ni ongezeko kutoka wanafunzi 4,000 waliopata mikopo mwaka uliopita. Serikali imeongeza bajeti ya mikopo kutoka Shilingi bilioni 30 mwaka uliopita hadi Shilingi bilioni 33.4 mwaka huu ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi wengi zaidi. Mikopo hii inatolewa kwa wanafunzi wa fani mbalimbali, zikiwemo sayansi ya afya, uhandisi, elimu, sheria, na biashara. Vigezo vya utoaji wa mikopo vinazingat...

MAJALIWA: WATOTO WAPELEKWE SHULE, AWATAKA WATENDAJI KUHAMASISHA HILO

Image
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa watendaji wa kata zote nchini kuungana na watendaji wa vijiji na mitaa ili kuhamasisha wazazi kuhusu umuhimu wa kuandikisha watoto wao wenye umri wa kwenda shule. Alisema kuwa ni jukumu la kila mzazi kuhakikisha mtoto wake anapata elimu bora, huku akisisitiza kuwa watoto wote wanapaswa kuanza masomo bila vikwazo. Akizungumza Desemba 22, 2024, katika viwanja vya shule ya sekondari ya Lion of Judah, wilayani Busega, mkoani Simiyu, Waziri Mkuu alisema: “Mtoto wa Kitanzania anatakiwa kwenda shule, na tunapaswa kuhakikisha kila mtoto anapata nafasi ya kuanzia chekechea, shule za msingi, na hadi sekondari.” Waziri Mkuu aliongeza kuwa suala la elimu ni la kipaumbele kwa serikali, na ni muhimu kuhakikisha watoto wote wanapewa nafasi ya kujiendeleza kimasomo. Aliwahimiza viongozi wa serikali za mitaa kufanya kazi kwa ushirikiano na wazazi ili kufanikisha lengo hilo. Katika kuhamasisha ushiriki wa wazazi, Majaliwa alieleza kuwa ni muhim...

WANAFUNZI WOTE WENYE UFAULU KATI YA 121 - 300 WAPANGIWA SHULE ZA SEKONDARI

Image
Serikali imehitimisha zoezi la uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Kwanza kwa mwaka 2025, likizingatia kigezo cha ufaulu wa mtahiniwa. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Mohamed Mchengerwa, Disemba 16, 2024, ametangaza rasmi kuwa wanafunzi wote waliopata alama kati ya 121 na 300 katika Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2024 wamechaguliwa na kupangiwa shule za sekondari za serikali. Aidha, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa jumla ya wanafunzi 974,332, wakiwemo wasichana 525,225 na wavulana 449,107, wamepangiwa shule. Hii ni sawa na asilimia 100 ya wanafunzi waliokuwa na sifa za kuchaguliwa. Wanafunzi waliofaulu wamepangiwa shule kwa kuzingatia makundi mawili makuu: 1. Shule za Sekondari za Bweni • Shule Maalum za Ufaulu wa Juu (Special Schools) • Shule za Amali za Kihandisi (Ufundi) • Shule za Bweni za Kitaifa Shule za bweni zimeundwa ili kuimarisha utaifa, kwa kuwachagua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi kw...

NAIBU WAZIRI PINDA AIPONGEZA ARITA KWA UBUNIFU WA TAARIFA ZA KIJIOGRAFIA

Image
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Geophrey Mizengo Pinda (Mb.), amepongeza ubunifu wa utafiti wa taarifa za kijiografia uliobuniwa na wahitimu wa Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA). Akizungumza katika mahafali ya 42 ya Chuo hicho yaliyofanyika Desemba 13, 2024, katika mtaa wa Ikulu, Kata ya Cheyo, Mkoani Tabora, Mhe. Pinda amesema kuwa ubunifu huo unaweza kuchochea maendeleo ya sekta ya ardhi nchini ikiwa utaratibu sahihi wa kuwawezesha wahitimu hao utaandaliwa. Aidha, Mhe. Pinda ametoa wito kwa halmashauri zote nchini kuvitumia vyuo vya Ardhi Tabora na Morogoro katika kupanga matumizi ya ardhi, kupima viwanja, na kuvimilikisha kisheria. Alisisitiza kuwa, “Ardhi isiyopimwa na isiyomilikishwa kisheria ni sawa na mtaji mfu.” Katika hotuba yake, Mhe. Naibu Waziri amewaasa wahitimu kuacha kabisa vitendo vya wizi, dhuluma, ubadhilifu, na kuomba au kupokea rushwa. Aliwataka kutumia ujuzi walioupata chuoni kwa manufaa ya umma, akisisitiza kuwa ardhi ni msingi wa maendeleo ...

BUNGE LA AUSTRALIA LAPIGA MARUFUKU MITANDAO YA KIJAMII KWA WATOTO CHINI YA MIAKA 16

Image
Bunge la Australia limepitisha sheria ya kwanza duniani inayozuia watoto chini ya miaka 16 kutumia mitandao ya kijamii kama TikTok, Facebook, na Instagram.  Aidha, Majukwaa yatakabiliwa na faini ya hadi dola milioni 50 za Australia ($33 milioni) kwa kushindwa kutekeleza marufuku hiyo. Sheria hiyo imepitishwa na Seneti kwa kura 34 dhidi ya 19 na Baraza la Wawakilishi kwa kura 102 dhidi ya 13. Majukwaa hayo yatapewa mwaka mmoja kujiandaa kabla ya adhabu kuanza kutekelezwa. Lengo kuu la kupitisha sheria hiyo ni kulinda watoto dhidi ya madhara ya mtandaoni, lakini wakosoaji wanahofia madhara yanayoweza kutokea, ikiwemo kutengwa kwa watoto walio katika mazingira magumu, athari kwa afya ya akili, na hatari kwa faragha ya watumiaji. Aidha Majukwaa hayataruhusiwa kushurutisha watumiaji kutoa hati za utambulisho zilizotolewa na serikali ikiwa ni pamoja na pasipoti au leseni za udereva, wala kudai kitambulisho cha kidijitali kupitia mfumo wa serikali.  Wayne Holdsworth, ambaye mtoto wak...

JINSI UTAFITI WA ULINZI ULIVYOLETA UVUMBUZI WA MITANDAO NA GPS

Image
Ubunifu na utafiti ni muhimu kwa nguvu ya taifa. Kadiri nchi inavyowekeza katika rasilimali na utaalamu ndivyo inavyozidi kuwa na nguvu. Ubunifu na utafiti wa kisayansi umekuwa ufunguo wa nguvu ya nchi. Kadiri nchi inavyowekeza rasilimali nyingi na uwezo, ndivyo nchi inavyozidi kuwa na nguvu.  Inashangaza, uvumbuzi mwingi ambao hutumiwa sana katika maisha yetu ya kila siku ulianzishwa kwa madhumuni ya kijeshi. Leo, ubunifu huu unaweza kupatikana karibu kila nyumba. Ingawa wengi bado hawajui asili yao. Mtandao sasa ni sehemu muhimu ya maisha ya kila siku na hatua kuu katika maendeleo ya kiteknolojia.  Mfano hai ni ARPANET ya Idara ya Ulinzi ya Marekani iliundwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 1969 ili kuunganisha vyuo vikuu, mashirika ya serikali na wakandarasi wa ulinzi nchini Marekani kupitia mtandao jumuishi.  Global Positioning System (GPS) GPS hutumiwa kwa usambazaji na ufuatiliaji wa trafiki na takriban ndege, meli na watu wote ulimwenguni kote, isipokuwa Uchina.  G...

WANAFUNZI NA WAFANYAKAZI WA KIGENI KUFUKUZWA MAREKANI

Image
"Rudini kwenye Kampasi': Vyuo Vikuu vya Amerika vyaonya Wanafunzi wa Kigeni huku hofu ya mpango wa Uhamiaji wa Trump kufukuza ikienea. Vyuo vikuu vya Marekani vinawataka wanafunzi wa kimataifa na wafanyakazi kurejea kabla ya muhula wa pili wa Rais mteule Donald Trump kuanza huku kukiwa na hofu ya kuwepo kwa sera kali za uhamiaji na kufukuzwa kwa wingi. Vyuo vikuu kote Marekani vimetuma barua pepe kwa wanafunzi na wafanyakazi wao wa kimataifa, na kuwashauri kurejea chuoni kabla ya Rais mteule Donald Trump kuanza muhula wake wa pili katika Ikulu ya White House, Januari 2025. Kwa mujibu wa ripoti na BBC, barua pepe hiyo inakuja kutokana na wasiwasi uliojitokeza kuhusu mpango wa Trump wa kufukuzwa kwa wingi, jambo ambalo huenda likaathiri maelfu ya wanafunzi wa kigeni. Ikimnukuu profesa katika Chuo Kikuu cha Colorado, ripoti hiyo ilisema kwamba wanafunzi wote wa kimataifa wana wasiwasi, kwani zaidi ya wanafunzi laki nne ambao hawajaandikishwa wamejiandikisha kwa elimu ya juu nchin...

SHULE ZA MSINGI 139 MBINGA KUPEWA KOMPYUTA

Image
 ðŸ“Œ *Kapinga asema lengo ni kuchochea kasi ya ukuaji wa Elimu* 📌 *Aweka Jiwe la Msingi ujenzi wa nyumba ya Mwalimu  Shule ya Mbungani* 📌 *Asema miradi ya maendeleo itawafikia wananchi wote bila kuangalia umbali* Naibu Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Vijana Mkoa wa Ruvuma Mhe.Judith Kapinga ameahidi kutoa kompyuta 139 katika Shule za Msingi 139 zilizopo Halmashauri ya wilaya ya Mbinga Vijijini ili kuchochea kasi ya ukuaji wa Elimu katika wilaya hiyo. Mhe. Kapinga ametoa ahadi hiyo Novemba 28, 2024 wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi kwenye ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu katika Shule ya Msingi Mbungani iliyopo Halmashauri ya wilaya ya Mbinga Vijijini. "Nitatoa kompyuta 139 ifikapo Januari 2025 ili zitumike katika Shule za Msingi 139 zilizopo Halmashauri ya Wilaya Mbinga Vijijini kwa lengo la kuendelea kuchochea kasi ya ukuaji wa maendeleo ya Elimu nchini."  Amesema Mhe. Kapinga Aidha, pamoja na kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa nyumba ya Mwalimu katika Sh...

DKT. SAMIA AWATUNUKU KAMISHENI MAAFISA WANAFUNZI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewatunuku Kamisheni pamoja Shahada ya Sayansi ya Kijeshi (BMS), Maafisa wanafunzi Kundi la 05/21 katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani Arusha.  

DKT. SAMIA AWATAKIA KHERI WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 11 Novemba 2024, amewatakia kila la kheri wanafunzi wote wa Kidato cha Nne wanapoanza  Mtihani wa Kuhitimu (CSEE) leo.  Aidha Dkt. Samia kupitia mtandao wake wa X anawaombea utulivu na mafaniko katika hatua hii muhimu ya watahiniwa wote kujiandaa kushiriki vyema kwenye nguvu kazi ya familia, jamii na Taifa kwa ujumla. "Mafanikio yenu katika hatua hii yatakuwa pia faraja kwa waalimu, wazazi na Watanzania wote ambao kupitia ulipaji kodi na utunzaji wa amani na utulivu wa nchi yetu mnaiwezesha  Serikali kuendelea kutekeleza mipango tunayojiwekea, ikiwemo kutoa elimu bure kuanzia Darasa la Kwanza hadi Kidato cha Sita, na kazi mpya tuliyoanza ya kuboresha mfumo wetu wa elimu ili uendane na mazingira na mahitaji ya sasa. Mwenyezi Mungu awaongoze na kuwasimamia." ameandika