DKT. SAMIA AWATAKIA KHERI WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 11 Novemba 2024, amewatakia kila la kheri wanafunzi wote wa Kidato cha Nne wanapoanza  Mtihani wa Kuhitimu (CSEE) leo. 


Aidha Dkt. Samia kupitia mtandao wake wa X anawaombea utulivu na mafaniko katika hatua hii muhimu ya watahiniwa wote kujiandaa kushiriki vyema kwenye nguvu kazi ya familia, jamii na Taifa kwa ujumla.


"Mafanikio yenu katika hatua hii yatakuwa pia faraja kwa waalimu, wazazi na Watanzania wote ambao kupitia ulipaji kodi na utunzaji wa amani na utulivu wa nchi yetu mnaiwezesha  Serikali kuendelea kutekeleza mipango tunayojiwekea, ikiwemo kutoa elimu bure kuanzia Darasa la Kwanza hadi Kidato cha Sita, na kazi mpya tuliyoanza ya kuboresha mfumo wetu wa elimu ili uendane na mazingira na mahitaji ya sasa.


Mwenyezi Mungu awaongoze na kuwasimamia." ameandika

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA