NAIBU WAZIRI PINDA AIPONGEZA ARITA KWA UBUNIFU WA TAARIFA ZA KIJIOGRAFIA

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Geophrey Mizengo Pinda (Mb.), amepongeza ubunifu wa utafiti wa taarifa za kijiografia uliobuniwa na wahitimu wa Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA).


Akizungumza katika mahafali ya 42 ya Chuo hicho yaliyofanyika Desemba 13, 2024, katika mtaa wa Ikulu, Kata ya Cheyo, Mkoani Tabora, Mhe. Pinda amesema kuwa ubunifu huo unaweza kuchochea maendeleo ya sekta ya ardhi nchini ikiwa utaratibu sahihi wa kuwawezesha wahitimu hao utaandaliwa.


Aidha, Mhe. Pinda ametoa wito kwa halmashauri zote nchini kuvitumia vyuo vya Ardhi Tabora na Morogoro katika kupanga matumizi ya ardhi, kupima viwanja, na kuvimilikisha kisheria. Alisisitiza kuwa, “Ardhi isiyopimwa na isiyomilikishwa kisheria ni sawa na mtaji mfu.”


Katika hotuba yake, Mhe. Naibu Waziri amewaasa wahitimu kuacha kabisa vitendo vya wizi, dhuluma, ubadhilifu, na kuomba au kupokea rushwa. Aliwataka kutumia ujuzi walioupata chuoni kwa manufaa ya umma, akisisitiza kuwa ardhi ni msingi wa maendeleo ya kila Mtanzania.


Katika chuo hicho jumla ya wahitimu 1,097 wametunukiwa Astashahada na Stashahada katika fani mbalimbali zikiwemo:

Urasimu Ramani

Usimamizi wa Ardhi

Sanaa, Ubunifu na Uchapaji

Usimamizi wa Mazingira

Mifumo ya Tehama


Mahafali haya yanaonesha mchango mkubwa wa Chuo cha Ardhi Tabora katika kuzalisha wataalam muhimu kwa maendeleo ya sekta ya ardhi nchini.


 

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA