MBIO ZA MWENGE DAR ES SALAAM
RAS RUGWA APOKEA MWENGE WA UHURU KUTOKA MKOA WA PWANI
*- Ataja ratiba ya Mwenge kukimbizwa Dar es Salaam*
*-Asisitiza Umuhimu wa Mwenge huu, Kauli Mbiu na Ujumbe wake*
*- Ataja thamani ya Miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru*
*-Akabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Wilaya Kinondoni ambapo DC huyo akiri kuupokea na kuukimbiza katika Wilaya yake*
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam *Ndg. Hassan Rugwa* amepokea Mwenge wa Uhuru Leo tarehe 10 Aprili 2022 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Bunju "A" ukitokea Mkoa wa Pwani
Baada ya kuupokea Mwenge huo wa Uhuru *Ndg. Hassan Rugwa* ametaja ratiba ya ukimbizwaji wa Mwenge katika Mkoa wa Dar es Salaam kuwa tarehe 10/05/2022 Utakimbizwa Kinondoni, tarehe 11/05/2022 Utakimbizwa Ubungo, tarehe 12/05/2022 Ilala, tarehe 13/05/2022 Kigamboni na kumalizika Temeke tarehe 14/05/2022 ambapo tarehe 15/05/2022 utakabidhiwa *Mkoa wa Kusini Pemba*
Aidha *Katibu Tawala* amesisitiza Umuhimu wa Mwenge wa Uhuru wa 2022 unaosisitiza Sensa ya Watu na Makazi chini ya Kauli Mbiu *" Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo; Shiriki Kuhesabiwa tuyafikie Maendeleo ya Taifa"* na Ujumbe wa Kudumu wa Mbio za Mwenge kuhusu Mapambano dhidi ya VVU/ UKIMWI, Malaria, Dawa za Kulevya, Lishe na Rushwa
*Ndg. Hassan Rugwa* amesema jumla ya *Miradi 28* yenye thamani ya *Shilingi Bilioni 16. 4* itapitiwa na Mwenge wa Uhuru ambapo Miradi hiyo ipo iliyokamilika na iliyopo katika hatua mbalimbali za utekelezaji
Hata hivyo *Katibu Tawala* ameukabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni *Mhe. Godwin Gondwe* ambaye amekiri kuupokea na kuukimbiza katika Wilaya yake ya Kinondoni
*MWENGE OYEEEEEE*

Comments