DKT SAMIA AMKUMBUKA IGP MSTAAFU SAID MWEMA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania- (IGP) mstaafu, Said Ally Mwema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Magazeti ya Serikali Tanzania (TSN).
Aidha IGP mstaafu Mwema anachukua nafasi ya Hab Mkwizu aliyemaliza muda wake. Taarifa za uteuzi huo zimetolewa leo Novemba 27, 2024 na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga.

Comments