DKT. SAMIA AMTEUA DKT. MPOKI KUWA BOSI MPYA MOI


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali leo nchini.


Aidha, amemteua Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI).


Pia amemteua Bi. Joyce Gideon Mapunjo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF). Bi. Mapunjo anachukua nafasi ya Mhandisi Musa Iyombe ambaye amemaliza muda wake.


Taarifa za uteuzi huo zimetolewa leo 02 Disemba 2024 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga.

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA