RAIS MWINYI: MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAMELETA MAFANIKIO MAKUBWA


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Mapinduzi ya Zanzibar yameleta mafanikio makubwa kwa wananchi wa Zanzibar, yakiwemo kujenga umoja, amani, na usawa miongoni mwa wananchi wote.


Akizungumza leo Januari 12, 2025 ikiwa ni siku ya maadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika kwenye uwanja wa Gombani, Pemba, Dkt. Mwinyi alitaja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na:

1. Mageuzi ya kiuchumi – Kuimarisha upatikanaji wa mapato na kudhibiti matumizi yake.

2. Miundombinu – Kuimarisha barabara, viwanja vya ndege, sekta ya michezo, afya, umeme, na maji.

3. Ustawi wa kijamii – Kuimarisha biashara, huduma za afya, na kuhakikisha utawala bora na demokrasia.


Aidha, Rais Mwinyi aliwasihi Wanazanzibari kutumia maadhimisho haya kama kumbukumbu ya ushindi wa kujikomboa kiuchumi, kisiasa, na kijamii. Pia aliwataka kuendelea kuwakumbuka waasisi wa Mapinduzi, akiwemo Hayati Abeid Amani Karume na viongozi wenzake.


Kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka huu, Rais Mwinyi amewataka Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla kushiriki kwa amani na utulivu huku akisisitiza vyombo vya mamlaka kusimamia uchaguzi kwa haki na usawa.

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA