RONALDO NA SAUDI WAZINDUA DAU LA TRILIONI 34.5 KUNUNUA MAN UNITED


Nguli wa Manchester United, Cristiano Ronaldo, ameungana na Mwana Mfalme wa Saudi Arabia kuzindua dau la pauni bilioni 11.5 sawa na fedha za kitanzania trilioni 34.5 kwa ajili ya kuinunua klabu hiyo.


Katika mahojiano maalum, Ronaldo alieleza maono yake kwa klabu hiyo akisema:

“Ninaamini huu ni wakati mwafaka kwangu kuwekeza, hasa na washirika sahihi. Manchester United ina nafasi ya kipekee moyoni mwangu. Changamoto za sasa za klabu, zinazosababishwa na usimamizi mbovu, ni changamoto tunayotaka kushughulikia kwa pamoja. Tunataka kuirejesha Manchester United katika hadhi yake ya zamani.”


Tangazo hilo limewaacha mashabiki wakiwa na mshtuko lakini pia furaha tele. Wengi wanaamini kuwa mchanganyiko wa mapenzi ya Ronaldo kwa klabu hiyo na msaada wa kifedha wa Saudia utahakikisha mustakabali mzuri wa klabu hiyo, na kufungua njia kwa zama mpya za mafanikio.

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA