TIKTOK YAPIGWA MARUFUKU KATIKA NCHI MBALIMBALI 9
TikTok, jukwaa maarufu la video, leo jumapili Januari 19, 2025 limepigwa marufuku kwa kusitisha rasmi matumizi katika baadhi ya nchi kutokana na masuala ya usalama na udhibiti wa mtandao. Nchi zilizochukua hatua hii ni pamoja na: • Afghanistan
• China
• India
• Iran
• Yordani
• Kyrgyzstan
• Korea Kaskazini
• Somalia
• Uzbekistan
• Marekani
Nchi nyingi zimetaja masuala kama usalama wa data, ushawishi wa kisiasa, na athari za kijamii kama sababu za kupiga marufuku matumizi ya TikTok, huku baadhi zikidai kwamba inahatarisha usalama wa kitaifa. Hata hivyo, jukwaa hili bado linapokelewa vizuri katika baadhi ya maeneo, likihusishwa na uhamasishaji wa ubunifu na biashara kwa watumiaji.

Comments