TRUMP AKOMESHA UPUUZI WA MAPENZI YA JINSIA MOJA, ASEMA NDIYO CHANZO CHA MOTO LOS ANGELES


Baada ya Donald John Trump kuapishwa jana kuwa Rais wa Marekani, alitangaza msimamo mkali dhidi ya mapenzi ya jinsia moja, akisema anatambua jinsia mbili tu: mwanaume na mwanamke. Alisema jinsia nyingine ni masuala binafsi ambayo hayapaswi kuwekwa wazi hadharani, akifananisha hali hiyo na changamoto zinazowakumba walemavu wengine.


Trump aliendelea kusema kuwa mtu yeyote atakayekutwa akipiga busu mwanaume mwenzake au mwanamke mwenzake hadharani atachukuliwa hatua kali za kisheria. Aidha, alitangaza kuwa watengenezaji wa filamu zinazohusiana na mapenzi ya jinsia moja watalazimika kulipa ushuru wa ziada kwa maudhui hayo.


Ikumbukwe kuwa mapenzi ya jinsia moja yalipewa nguvu kubwa chini ya aliyekuwa Rais wa Marekani, Joseph Robinette Biden Jr., huku aliyekuwa Makamu wake, Kamala Devi Harris, akihimiza ajenda hiyo barani Afrika. Harris alihusishwa na kampeni za kueneza maadili hayo kupitia mikutano mbalimbali barani humo, ikiwemo usambazaji wa vitabu vyenye maudhui yanayokinzana na maadili ya familia za Kiafrika.


Katika hotuba yake ya uzinduzi, Trump alieleza kwamba hatua hizo zinahitajika ili kulinda kizazi kijacho dhidi ya mmomonyoko wa maadili, akisisitiza kuwa sera za Biden zilichangia kushamiri kwa hali hiyo kupitia mipango yake ya kimataifa isiyo na mipaka.


Trump ameahidi kurejesha maadili ya kimila na kidini kama nguzo muhimu ya maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla, akisema kuwa maadili hayo ndiyo msingi wa kujenga familia imara na jamii yenye maelewano.

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA