TRUMP AWAPIGA MARUFUKU BRICS KUACHANA NA DOLA, ATISHIA KUWEKA USHURU MKUBWA


 

Rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump, ameonya vikali kundi la mataifa ya BRICS dhidi ya jaribio lolote la kuachana na matumizi ya Dola ya Marekani (USD) katika biashara za kimataifa. Trump ametangaza kuwa ikiwa BRICS itaendelea na mpango wa kuanzisha sarafu mpya au kuunga mkono sarafu nyingine badala ya dola, basi Marekani itaweka ushuru wa 100% kwa bidhaa zao.


Trump amesema kuwa hatakubali Marekani kusimama tu na kushuhudia BRICS ikihatarisha nafasi ya dola katika uchumi wa dunia. Ameongeza kuwa mataifa yanayoonekana kuwa “ya uhasama” lazima yahakikishe hayataunda sarafu mpya ya BRICS au kusaidia sarafu nyingine kuchukua nafasi ya dola, vinginevyo yatakabiliwa na vikwazo vikali vya kiuchumi.


“Hakuna nafasi kwamba BRICS itachukua nafasi ya dola ya Marekani katika biashara ya kimataifa au mahali pengine popote. Taifa lolote litakalojaribu, lijiandae kukabiliana na ushuru mkali na kusema kwaheri kwa soko la Marekani,” amesema Trump.


Kauli hii imekuja wakati ambapo mataifa ya BRICS, yanayojumuisha Brazil, Russia, India, China, na South Africa, yanaendelea kujadili mbinu za kuimarisha matumizi ya sarafu zao katika biashara za kimataifa, jambo linaloonekana kama changamoto kwa ustawi wa dola ya Marekani.

Comments

Popular posts from this blog

RAIS SAMIA AHIMIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

SERIKALI YAHAKIKISHA USAFIRI BORA BRT AWAMU YA PILI

RAIS WA CABO VERDE ASISITIZA UTAWALA BORA NA ULIPAJI FIDIA KWA AFRIKA KATIKA UFUNGUZI WA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA YA AFRIKA JIJINI ARUSHA