Posts

MAHUSIANO YA AFRIKA NA URUSI

Image
  Kihistoria uhusiano wa Urusi na Afrika ulikuwa tofauti na wakoloni wengine wa Kiafrika kama vile Britain France Portugal na Belgium. Ukweli kwamba Urusi haikujaribu kuitawala Afrika na kwamba soviet iliunga mkono mapambano dhidi ya ukoloni Barani Afrika inaipa nchi hiyo sifa ya kuwa mshirika wa kutegemewa. Wakati wa enzi ya vita baridi muungano wa Soviet ulitoa msaada wa kidiplomasia, kiuchumi na kijeshi kwa nchi mbalimbali za Afrika. Pia ilitoa msaada kwa mapambano ya ukombozi wa Kitaifa Barani Afrika kama sehemu ya malengo ya sera ya kigeni ya katiba ya Soviet. Gobachev, Mikail kiongozi wa Mwisho wa Soviet, wakala wa CIA aliyetumwa na Marekani kuvunja USSR. Baada ya kuvunjika kwa Soviet mnamo Desemba 1991 Urusi ilikuwa dhaifu kiuchumi, kwa hivyo haikutaka kujihusisha na Afrika bali kuimarisha uchumi wake. *KWANINI TUNAHITAJI URUSI?* 1. Urusi inashughulikia sehemu kubwa ya Ulaya na Asia ya kaskazini 2. Idadi ya watu 3. Ni nguvu kuu ya nyuklia. 4. Ni muuzaji mkubwa zaidi wa gesi ...

MANENO YA PAPA FRANCIS KUHUSU YANAYOENDELEA UKRAINE NA RUSIA

Image
  KAULI YA PAPA FRANCIS DHIDI YA UKRAINE NA RUSIA  Kufuatia vitendo vya kuashiria vita vinavyoendelea baina ya Urusi na Ukraine, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis amesema hatari ya vita ilmesababisha maumivu makali moyoni mwake. Ametoa wito kwa watu wote kutumia siku ya Machi 2, 2022 ambayo ni Jumatano ya Majivu, kufunga na kuiombea Ukraine. Ripoti zinaonesha tayari Russia imeanza kuishambulia Ukraine. Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Dmytro Kuleba amesema watashinda vita hiyo. Nukuu ya papa  “Call to prayer and fasting requested by Pope Francis for March 2, 2022  Pope Francis: "I have great pain in my heart over the worsening situation in Ukraine," "I would like all those who have the political responsibility to make a serious examination of conscience before God, who is the God of peace and not of war... He wants us to be brothers and not enemies. I pray that all parties involved will refrain from any action that will cause even more s...

KURASA ZA MBELE ZA MAGAZETI YA LEO TAREHE 25/2/2022

Image
  Kurasa za mbele za magazeti ya leo tarehe 25/2/2022

KAULI YA CHINA KWA UKRAINE NA URUSI

Image
  China imesema inafuatilia kwa ukaribu mzozo kati ya Urusi na Ukraine na kuilaumu Marekani kuwa inachochea mzozo huo ili iendelee kuuza silaha za kivita kwa Ukraine "Tunaziomba pande zote mbili kufungua milango ya mazungumzo ya amani badala ya kuendeleza vurugu" Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa China, Hua Chunying, amesema  "Marekani inachochea vita na mzozo wa Urusi na Ukraine kwa muda mrefu sasa huku ikinufaika na mzozo huo kwa kuiuzia Ukraine silaha zenye thamani ya zaidi ya USD Bilioni 1.5, sio sawa kuwanyooshea vidole Watu kwa moto uliouchochea mwenyewe"  "Baadhi ya Vyombo vya Habari vinatumia neno 'Uvamizi' kwamba Urusi imeivamia Ukraine lakini Vyombo hivi vilitumia neno gani wakati Marekani ilipofanya uvamizi kama huo na vitendo vya kivita dhidi ya Afghanistan na Iran bila kibali cha kisheria kutoka Umoja wa Mataifa!?" Kauli hiyo ya China dhidi ya mataifa hayo ni ya kutaka amani.

ALICHOSEMA KANALI DOUGLAS MACGREGORY DHIDI YA UKRAINE NA URUSI

Image
  Colonel Douglas Macgregor, afisa mstaafu wa jeshi la Marekani amevunja ukimya kwa kusema kuwa Marekani ina nafasi ya kuepusha vita na Putin (Russia). Jambo la kwanza wanalopaswa kufanya Wamarekani ni kukiri na kukubaliana na nukta ya msingi ya Putin (Russia), ambayo serekali ya Russia imeiweka wazi kwa zaidi ya miaka 25 sasa. Nukta yenyewe ni kuwa Russia hawataki majeshi ya Marekani, mizinga ya Marekani, na majeshi ya NATO kwenye mpaka wake na Ukraine  (Mashariki ya Ukraine kwenye majimbo yaliyotangazwa huru na Putin). Colonel Douglas akaendelea kusema: Kiukweli kabisa hata sisi Wamarekani hatukuyataka majeshi ya Russia na mizinga yake ndani ya Cuba, Putin naye hataki mambo hayo mashariki mwa Ukraine. Lazima tukubali madai hayo. Tuache kujifanyisha kuwa madai hayo hayana maana (ni ya kipuuzi). Zaidi ya hapo Colonel huyo kasema Marekani haina uwezo wa kumfanya chochote Putin dhidi ya uvamizi wake.

TISHIO LA KIVITA KATI YA UKRAINE NA URUSI

  RAIS wa Urusi Vladimir Putin ametangaza operesheni ya kijeshi katika eneo la Donbas nchini Ukraine Akitoa tamko hilo katika hotuba ya televisheni leo  asubuhi amewataka wanajeshi wa Ukraine waliopo katika eneo la mapigano mashariki mwa Ukraine kuweka silaha chini na kurejea majumbani mwao. Aidha Saa chache baadaye milipuko ilisikika katika miji ya Odessa, Kharkiv, Kramatorsk, Mariupol and Kyiv Nchini Ukraine. Naye Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema operesheni ya Russia imelenga kambi za jeshi za Taifa hilo hata hivyo Bunge la Ukraine limepitisha azimio la nchi hiyo kuwa katika hali ya hatari kwa siku 30 kutokana na mzozo uliopo kati ya Nchi hiyo na Urusi. Mamlaka nchini humo zimeruhusiwa kuzuia raia kutoka, kuzurura na kuzuia Mikutano ya Vyama vya Siasa na Taasisi kwa maslahi ya Taifa. Pia, Serikali imewalazimisha kujiunga na jeshi wanaume wote waliofikia umri wa kwenda vitani. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres amemtaka Rais wa Urusi, Vladimir Pu...

MAGAZETI YA LEO TAREHE 24/2/2022

Image
 Karibuni kujua kilichojiri katika kurasa za mbele za magazeti ya leo tarehe 24/2/2022

MAGAZETI YA LEO TAREHE 23/2/2022

Image
 Kurasa za mbele za magazeti ya leo tarehe 23/2/2022

RAIS SAMIA ATAKA JESHI LA POLISI KUSHIRIKIANA NA WANANCHI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu Hassan ameliagiza jeshi la polisi kushirikiana na wananchi na viongozi mbali mbali katika kukabiliana na mauaji na watu kujiua. Rais Samia ametoa agizo hilo wakati akihutubia kwenye sherehe za Jubilee ya miaka 25 ya utumishi wa Askofu Severine Niwemugizi zilizofanyika katika viwanja vya posta, Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera. Rais Samia amesisitiza kwamba harakati hizo lazima ziwe shirikishi kwani viongozi wa mitaa na vijiji ndio wanaofahamu watu wao ambao wamekuwa moja ya chanzo cha mauaji hayo. Takwimu zinaonesha kwamba mwaka 2020 wilaya ya Ngara pekee kulikuwa na matukio 22 ya mauaji na mwaka 2021 kulikuwa na matukio 21 huku kukiwa na matukio matatu ya watu kujiua mwaka 2020 na mawili mwaka 2021. Ripoti za uchunguzi huonyesha sababu za ongezeko la matukio hayo ni kutokana na wivu wa kimapenzi, kuwania mali, kulipiza visasi, imani za kishirikina, ugomvi wa kifamilia pamoja na msongo wa mawazo. Rais Samia ameshaliagiza jeshi...

Magazeti ya leo tarehe 22/2/2022

Image
Kurasa za mbele za magazeti ya leo Tanzania